Last Update :   2 May 2012 (Jumatano)
    11 Jumadal Aakhar (Mfungo Tisa) 1433 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!
 
 
  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5


Dondoo za wiki

Wasia
“Wasia”, ni neno linalo beba maana mbili; maana ya kilugha (isiyo rasmi) na ile ya kisheria (maana rasmi). Twendapo na maana ya “Wasia” katika lugha, neno “Wasia” hutumika katika lugha kwa maana ya “kufikisha”. Ama “Wasia” katika sharia ni: Utoaji hiba wa haki ya mali, unao unganishwa na kipindi cha baada ya mauti ya mtoaji.
Na utoaji hiba huu umeitwa “Wasia”, kwa sababu yule anaye usia (Mtoa hiba) huwa kwa utoaji wake huo ameiunga kheri ya marejeo yake (Akhera) na kheri ya Dunia yake. Endelea ....


Kuunga undugu...Inaendelea
Katika jamii yenye kupendana kwa upendo wa Allah, jamii inayo kusanywa na matukufu ya Uislamu. Katika jamii hiyo, udugu wa imani hukaa mahala pa udugu wa nasabu/damu, na pengine kiunganishi cha imani kikakishinda kile kiunganishi cha damu. Na lililo la haki kusemwa ni kwamba, kamba za udugu kwa ajili ya Allah, ndizo ambazo zilizo wakusanya Waislamu kwa mara ya kwanza na zikaiasisi Dola ya Kiislamu na zikaipeperusha bendera ya Uislamu. 
Endelea .....


Waraka wa Sayyidna Uthman kwa Waislamu
Kufuatia mzingiro mkali ambao haukumpa hata fursa ya kutoka kuwaswalisha Waislamu swala za jamaa, Sayyidna Uthman-Allah amuwiye radhi-akamuamrisha Uthman bin Abdillah bin Abbas akawaongoze watu katika ibada ya Hijja, akasema: Kupigana na (waasi) hawa kunapendeza mno kwangu kuliko kwenda kuhiji (kwa sasa). Basi akamtilia mkazo katika amri hiyo mpaka akatii, akatoka kwenda kuwahijisha watu na akamuandikia waraka akiwafahamisha Waislamu juu ya kadhia yake. Endelea ...


Mazungumzo baina ya Mitume na kaumu yao ...Inaendelea
Na mahala pa nne tunawaona washirikina wakimwambia Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie: Ewe Muhammad! Sisi katu hatutakuamini wewe mpaka na sisi tushushiwe wahyi kama unavyo shushiwa wewe. Qur-ani inawarudi ikiwabainishia ya kwamba utume ni hiba/tunu ambayo Allah Ataadhamiaye humtunukia amtakaye miongoni mwa waja wake. Na kwamba wahyi hauteremshwi ila kwa mitume walio teuliwa na kukhitariwa na Allah-utakati wa mawi ni wake-kuichukua risala yake na kuifikisha da’awa yake.  Endelea ...

 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

“HEBU HUKUWAONA WALE WALIO IBADILISHA NEEMA YA ALLAH KWA KUFURU, NA WAKAWAFIKISHA WATU WAO KWENYE NYUMBA YA MAANGAMIZO? NAYO NI JAHANNAMU! MAOVU YALIYOJE MAKAAZI HAYO!” [14:28-29]

 

Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Si mbora wenu, yule aliye iacha Dunia yake kwa ajili ya (kuitafuta) Akhera yake, wala yule aliye iacha Akhera yake kwa ajili ya Dunia yake mpaka avipate vyote viwili. Kwa sababu Dunia ni njia ya kuifikia Akhera na wala msiwe mzigo mzito kwa watu”. Ibn Asaakir-Allah amrehemu.

 

Katazo la Wiki

Kwa nini lakini, kwa nini utende dhambi kisha umuombe maghufira Mola wako, halafu tena urejee kuitenda dhambi ile ile uliyo itakia maghufira?! Huo ni mchezo mbaya, tena wenye mwisho mbaya, tahadhari! Mtume-Rehema na Amani zimshukie-anasema: “Mtaka maghufira ya dhambi na ilhali anaendelea na dhambi hiyo, huyo ni kama mwenye kumcheza shere Mola wake”.

 

Swali la Wiki

SWALI: Mwanamke mwenye janaba anapo oga, je analazimika kuosha nywele zake mpaka maji yaifikie ngozi ya kichwa?

JIBU: Kuoga kwa ajili ya janaba au mengineyo yanayo pasisha josho, kunapasa ndani yake kuyafikisha maji kwenye maoteo/mameleo ya nywele, iwe ni kwa mwanamke au mwanamume, kwa mujibu wa kauli yake Allah Ataadhamiaye: “...NA MKIWA NA JANABA, BASI OGENI...” [05:06]
Na wala hakumjuzii kuosha juu ya nywele tu, bali hapana budi maji yafike kwenye mashina ya nywele, mpaka kwenye ngozi ya kichwa.
Allah ndiye Mjuzi mno.

 


| Tuandikie |

: