|
SWALI: Mwanamke mwenye janaba
anapo oga, je analazimika kuosha nywele zake
mpaka maji yaifikie ngozi ya kichwa?
JIBU: Kuoga kwa ajili ya janaba au mengineyo
yanayo pasisha josho, kunapasa ndani yake
kuyafikisha maji kwenye maoteo/mameleo ya nywele,
iwe ni kwa mwanamke au mwanamume, kwa mujibu wa
kauli yake Allah Ataadhamiaye: “...NA MKIWA NA
JANABA, BASI OGENI...” [05:06]
Na wala hakumjuzii kuosha juu ya nywele tu, bali
hapana budi maji yafike kwenye mashina ya nywele,
mpaka kwenye ngozi ya kichwa.
Allah ndiye Mjuzi mno.
|