|
SWALI: Nini hukumu ya mwanamke kumuingilia mkewe naye
akiwa hedhini?
JIBU: Mwanamume kumuingilia mkewe katika hali ya hedhi,
ni jambo lililo harimishwa kwa nassi (nukuu) ya Qur-ani na Sunna.
Allah Ataadhamiaye anasema: “NA WANAKUULIZA JUU YA HEDHI. WAAMBIE,
HUO NI UCHAFU. BASI JITENGENI NA WANAWAKE WAKATI WA HEDHI. WALA
MSIWAINGILIE MPAKA WATWAHIRIKE...”. [02:222]
Mwanamume atakapo thubutu kumuingilia mkewe ndani ya
kipindi cha hedhi, kumemlazimu kuleta toba na kutokurudia tena
kitendo hicho na pia amewajibikiwa na kafara, nayo ni kutoa dinari
moja au nusu ya dinari. Hilo ni kwa mujibu wa hadithi ya Ibn
Abbas-Allah amuwiye radhi-katika kadhia ya yule aliye muingilia mkewe
naye akiwa hedhini, alisema: “Atoe sadaka ya dinari moja au nusu
dinari”. Ahmad, Abu Daawoud, Tirmidhiy & Nasaai-Allah
awarehemu.
Na muradi wa “dinari” ni tola (mithqaali) moja ya
dhahabu, akitoipata basi inatosha thamani yake katika fedha.
Allah ndiye Mjuzi mno.
|