Last Update :  05 May 2008 (Jumatatu)
29 Rabiul-Thani(Mfungo saba) 1429 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!
 
 
  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5


Dondoo za wiki

 Sunna za Posa
Kunasuniwa kwa mposaji au wakili wake, kutanguliza khutuba kabla ya kuleta tamko la posa na kabla ya kifungo cha ndoa. Aianze hiyo khutba kwa kumuhimidi Allah na kisha kumswalia Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie. Hayo ni kwa mujibu wa hadithi isemayo: “Kila jambo jema lisilo anzwa kwa kumuhimidi Allah, basi jambo hilo ni lenye kukatika (baraka)”. Ibn Maajah [1894]-Allah amrehemu. Baada ya kumuhimidi Allah, ausie kumcha Allah, halafu ndipo ayadhihirishe matashi yake kwa kusema: Nimekujilieni kumposa binti yenu. Endelea .....


Kujua kuwa maisha ya mafanikio ni mafupi sana 
Mtu mweledi anajua kwamba maisha yake ya sawa sawa, maisha ya mafanikio na utulivu, ni maisha mafupi sana. Kwa hivyo basi, kwa kuukiri na kuujua ukweli huu, anajua ya kwamba haitakikani kwake kuzidi kuyafupisha kwa kuwa na wahaka/huzuni na jakamoyo. Kwani yote hayo ni kinyume na maisha ya sawa sawa, kwa ajili hiyo huionea unyimi sehemu kubwa ya maisha yake kuporwa na wahaka/huzuni/jakamoyo. Na katika hili hapana tofauti baina ya mja mwema na yule aliye muovu. Lakini muumini yeye katika wasifu huu, ana fungu toshefu la Duniani na Akhera. Endelea .....


Khabari za Kandah
Watu wa Kandah walikuwa wameritadi katika zama za Nabii wa uwongo; Al-Aswad. Waliliritadi kwa sababu ya yaliyotokea baina yao na gavana Ziyaad Ibn Labeed katika kadhia ya faradhi ya Zakah. Kadhia hii ilitokana na makadirio ya zakah yaliyo kosewa na ikachochewa na watu wa kabila la Amrou Ibn Muawiyah hapo Kandah. Kwa sababu ya uritadi wao huu, ndipo gavana Ziyaad akakata shauri la kuwapiga vita, akawapiga na kuwashinda.   Endelea ...


Sababu za kutofautiana maoni baina ya watu
Ikhtilafu/tofauti baina ya watu katika mambo/masuala ya dini yao na katika kadhia za Dunia yao, ni suala kongwe, la tangu na tangu. Na tofauti hizi zitaendelea kuishi na kusalikia miongoni mwao mpaka kumalizika kwa Dunia na vyote vilivyomo humo. Ukweli huu usio kanushika na akili pevu na hakika hii isiyo katalika, imekokotezwa na kusisitizwa na Qur-ani Tukufu kupitia aya zake nyingi tu. Miongoni mwa hizo ni kauli yake Ataadhamiaye: “NA MOLA WAKO MLEZI ANGELI PENDA ANGELI WAFANYA WATU WOTE WAKAWA UMMA MMOJA. LAKINI HAWAACHI KUKHITALIFIANA ISIPO KUWA WALE AMBAO MOLA WAKO MLEZI AMEWAREHEMU. NA KWA HIYO NDIO ALLAH AMEWAUMBA...” [11:118-119]
  Endelea ...

 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

“WALE WALIO AMINI NA WAKATENDA MEMA WATAKUWA NA RAHA NA MAREJEO MAZURI”. [13:29]

Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Kwa yakini kila kitu kina hakika yake na mja hatafikilia hakika ya imani mpaka atambue kwamba lililo msibu halikuwa limkose (lisimsibu). Na lililo mkosa halikuwa limsibu (ndio maana limemkosa)”. Ahmad-Allah amrehemu.

Katazo la Wiki

Ni haki yako kula, kunywa, kuvaa na kuishi mahala pazuri kutokana na neema za Allah alizo kuneemesha. Lakini kwa nini mtu mmoja wewe ubadili nguo kutwa mara tatu, ilhali kuna waendao uchi kwa kukosa nguo?! Kwa nini ule na kutupa jaani na ilhali wako washindao na kulala njaa?! Hiyo ni israfu ambayo Allah haipendi: “Kula, kunywa, uvae na utoe sadaka bila ya israfu wala maringo”. Ahmad-Allah amrehemu.

Swali la Wiki

SWALI: Ninashindwa kuoa kwa sababu za kimaada; sina kitu na mawimbi makubwa ya haja ya kutaka kuoa yananipiga, nifanyeje?

JIBU: Hakika kushindwa kwako kuoa kwa sababu ya kutokuwa na kitu, si sababu tosha ya kukupa uhalali wa kuwa na mpenzi nje ya ndoa. Bali kuwa na mpenzi wa nje kutakusababisha utumie gharama zaidi, na Mtume – rehema na amani zimshukie – anasema "Zinaa hurithisha ufakiri", na "mwenye kuoa ili ajihifadhi na madhambi, Mwenyezi Mungu atamhifadhi".

Allah ndiye Mjuzi mno. 


| Tuandikie |

: