|
SWALI: Nimeweka nadhiri kuvaa
Hijabu, lakini mazingira ya shule yanayo
nizunguka hayaruhusu, nifanyeje?
JIBU: Hijabu ambayo inamaanisha
kusitiri sehemu ya mwili wa mwanamke isiyo uso
na vitanga vya mikono yake, ni WAJIBU kwa kila
binti aliye fikia umri wa taklifu. Na kuweka
nadhiri ya kutekeleza wajibu, hakubadilishi
chochote katika wajibu huo. Bali tu ni kwamba
wajibu huo hurudufika umuhimu wake kwa sababu ya
nadhiri hiyo. Na kwa upande mwingine, hurudufika
pia madhambi ya kuzembea kuutekeleza wajibu huo.
Na wala nadhiri hiyo haina kafara itakayo
ondosha wajibu wa kuitekeleza kama unavyo
dhania. Na hakika si vinginevyo, kafara iliyo
wekwa na sheria na ambayo ni wajibu, ni pale mtu
anapo kwenda kinyume na yamini (kiapo) na
nadhiri inatofautiana na yamini kihukumu.
Madhehebu ya Ibn Abbas-Allah
amrehemu-na amefuatwa katika hayo na Jamuhuri ya
wanatafsiri, ni kwamba muradi/mapendeleo ya
“...ISIPO KUWA UNAO DHIHIRIKA...” ni uso na
vitanga vya mikono. Na zipo hadithi nyingi
zilizo thibiti zinazo yatia nguvu madhehebu
haya. Hii ndio hukumu ya Sheria kwa mukhtasari.
Allah ndiye Mjuzi mno. |