|
SWALI: Ninashindwa kuoa kwa
sababu za kimaada; sina kitu na mawimbi makubwa
ya haja ya kutaka kuoa yananipiga, nifanyeje?
JIBU: Hakika kushindwa kwako
kuoa kwa sababu ya kutokuwa na kitu, si sababu
tosha ya kukupa uhalali wa kuwa na mpenzi nje ya
ndoa. Bali kuwa na mpenzi wa nje kutakusababisha
utumie gharama zaidi, na Mtume – rehema na amani
zimshukie – anasema "Zinaa hurithisha ufakiri",
na "mwenye kuoa ili ajihifadhi na madhambi,
Mwenyezi Mungu atamhifadhi".
Allah ndiye Mjuzi mno. |