Last Update :  22Juni 2009 (Jumatatu)
  28 Jumadal-Akhar (Mfungo tisa) 1430 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!
 
 
  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5


Dondoo za wiki

Kufanya mahari ghali mno
Watu wengi huifanya mahari kama ni thamani ya mwanamke na wanadhania kwamba kuighalisha ni nembo ya utukufu wa familia yake. Ni kwa ajili/sababu hiyo basi, wanapita kiasi katika kiwango cha mahari na wanaighalisha katika kuifanya kubwa na nyingi ili kuonyesha thamani ya binti/muolewa. Na kuonyesha utukufu wa daraja/cheo cha familia yake na kujifakharisha kwa mabinti/wanawake wenzake katika shughuli ya harusi yake na samani za nyumba yake.Endelea .....


Ukweli...inaendelea
Watu wengi huifanya mahari kama ni thamani ya mwanamke na wanadhania kwamba kuighalisha ni nembo ya utukufu wa familia yake. Ni kwa ajili/sababu hiyo basi, wanapita kiasi katika kiwango cha mahari na wanaighalisha katika kuifanya kubwa na nyingi ili kuonyesha thamani ya binti/muolewa. Na kuonyesha utukufu wa daraja/cheo cha familia yake na kujifakharisha kwa mabinti/wanawake wenzake katika shughuli ya harusi yake na samani za nyumba yake.
 
Endelea .....


Uongozi wa Sa'd na wasia wa Sayyidna Umar
Lilipo mkusanyikia Amirul-Muuminina; Sayyidna Umar-Allah amuwiye radhi-jeshi kubwa, akatoka nalo baada ya kumkaimisha Sayyidna Aliy Bin Abi Twaalib uamiri wa Madina. Akaenda na jeshi mpaka Dhiraar; mahala nje kidogo ya Madina, wakapiga kambi hapo ilhali Waislamu hawajui makusudio wala muelekeo wake; je ataelekea Iraq au atabakia hapo? Sayyidna Uthman Bin Affan-Allah amuwiye radhi-akawa ndiye mtu wa kwanza kumuuliza juu ya harakati zake hizo. Nae akamjulisha makusudio/muelekeo wake, kisha akamuuliza je, yeye abakie Madina na kumtawalisha uongozi wa jeshi mtu mwingine au aliongoze jeshi yeye mwenyewe? Watu awaami; wasio na mamlaka yoyote wakamwambia: Enenda na utuchukue nasi pamoja nawe. Na watu khaasi; maalumu katika maswahaba wa Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-wakamshauri kubakia Madina.   Endelea ...


Kuheshimu rai ya wenye akili pevu ...Inaendelea
Kadhalika katika jumla ya mifano itoayo nuru ambayo inafahamisha ya kwamba mtu bora, ni yule anaye heshimu rai/maoni ya watu wenye akili pevu hata kama ni wa chini yake kidaraja. Na kwamba yeye anaweza kutwaa maoni yao hata kama yanapingana na maoni yake yeye. Miongoni mwa mifano hiyo, ni yale yaliyo tokea baina ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-na baadhi ya maswahaba wake..
  Endelea ...

 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

“NA KATIKA WATU, WAKO WASEMAO: TUMEMWAMINI ALLAH NA SIKU YA MWISHO, WALA WAO SI WENYE KUAMINI”. [02:08]

Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Chakula kibaya kilioje, ni kile  chakula cha karamu wanacho alikwa matajiri na kuachwa mafakiri. Na atakaye kataa mwaliko kwa yakini amemuasi Allah na Mtume wake”. Bukhaariy & Muslim-Allah awarehemu.

Katazo la Wiki

Allah Ataadhamiaye ndiye aliye kuumba wewe na akakurimu neema ya mali na ni Yeye huyo huyo ndiye aliye muumba ndugu yako na kwa hekima zake akamkirimu umasikini. Kwa nini basi umdharau, umkebehi, umnyanyase na hata kuthubutu kumuonea eti kwa sababu tu yeye ni masikini?! Acha, kwani huko ni kuutupa ufunguo wa Peponi kama alivyo sema Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie: “Kila kitu kina ufunguo (wake) na ufunguo wa Pepo ni kuwapenda masikini na mafakiri”. Ibn Laal-Allah amrehemu.

Swali la Wiki

SWALI: Nimeweka nadhiri kuvaa Hijabu, lakini mazingira ya shule yanayo nizunguka hayaruhusu, nifanyeje?

 

JIBU: Hijabu ambayo inamaanisha kusitiri sehemu ya mwili wa mwanamke isiyo uso na vitanga vya mikono yake, ni WAJIBU kwa kila binti aliye fikia umri wa taklifu. Na kuweka nadhiri ya kutekeleza wajibu, hakubadilishi chochote katika wajibu huo. Bali tu ni kwamba wajibu huo hurudufika umuhimu wake kwa sababu ya nadhiri hiyo. Na kwa upande mwingine, hurudufika pia madhambi ya kuzembea kuutekeleza wajibu huo. Na wala nadhiri hiyo haina kafara itakayo ondosha wajibu wa kuitekeleza kama unavyo dhania. Na hakika si vinginevyo, kafara iliyo wekwa na sheria na ambayo ni wajibu, ni pale mtu anapo kwenda kinyume na yamini (kiapo) na nadhiri inatofautiana na yamini kihukumu.

Madhehebu ya Ibn Abbas-Allah amrehemu-na amefuatwa katika hayo na Jamuhuri ya wanatafsiri, ni kwamba muradi/mapendeleo ya “...ISIPO KUWA UNAO DHIHIRIKA...” ni uso na vitanga vya mikono. Na zipo hadithi nyingi zilizo thibiti zinazo yatia nguvu madhehebu haya. Hii ndio hukumu ya Sheria kwa mukhtasari.

Allah ndiye Mjuzi mno.


| Tuandikie |

: