Last Update :  22 Mei 2013 (Jumatano)
   12 Rajab1434 AH

Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu  
Uliza Suala la dini
Jiunge  !!!


  Karibu kwenye Mtandao wa UISLAMU  

"Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba, Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! Ambaye amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui...." 96:1-5








Dondoo za wiki

Elimu yaMirathi
Elimu ya Mirathi katika Sharia: Hii ni mojawapo ya fani za elimu ya Fiq-hi inayo shughulika na suala zima la ugavi wa mirathi kwa upande mmoja. Na kwa upande wa pili inashughulika na hesabu kama nyenzo ya kufikisha kujua hisa/fungu la kila mwenye haki katika tarika (mali iliyo achwa na marehemu). Endelea ....


Utukufu wa nafsi (Kujiheshimu/hadhi ya mtu
Utukufu/ukubwa na ufalme/utawala juu wa waja, hiyo ni sifa ya Mola Mlezi wa waja, ambaye aliye umba na akaweka sawa; yaani aliye umba kila kitu na akajaalia uumbaji wote sawa sawa katika hukumu na kupangana. Na ambaye amekadiria na akaongoa; yaani na akakadiria kwa kila kitu kwa mujibu wa maslahi yake na anakiongoza. Na ambaye anapo dhihiri, hutenza nguvu; yaani hashindiki. Na ambaye anapo jionyesha, huingiwa na kiwewe wenye akili miongoni mwa watu, kwa sababu ya nuru za utukufu wake. Huyu aliye hodhi sifa hizi, ndiye aliye na utukufu/ukubwa na ufalme/utawala wa kweli juu ya waja.
.Endelea .....


Vita vya Swaffein...Inaendelea
Kipindi cha kutoingia vitani kilipo malizika, Sayyidna Aliy-Allah amuwiye radhi-akamuamuru mpiga mbiu kupiga mbiu (aseme): Enyi watu wa Shamu nyie! Amirul-Muuminina anakuambieni ya kwamba yeye alikupeni muda ili mpate kuichunga haki. Lakini nyinyi bado hamjauacha upotofu/uasi wenu na wala hamjaiitika haki. Na hakika mimi nimesha kutupieni ahadi yenu, hakika Allah hawapendi watu makhaini.   Endelea ...


Majadiliano na watu wa Kitabu...Inaendelea
Kudai kwao ya kwamba nyumba ya Akhera (pepo) ni yao wao peke yao na kwamba wasio wao miongoni mwa watu wengine hawana nafasi humo. Na Qur-ani tukufu ikayarudi madai yao hayo katika aya kadhaa, miongoni mwake ni kauli yake Allah Ataadhamiaye: “SEMA: IKIWA NYUMBA YA AKHERA ILIYOKO KWA ALLAH NI YENU TU BILA YA WATU WENGINE, BASI TAMANINI MAUTI KAMA NYINYI MNASEMA KWELI. WALA HAWAYATAMANI KAMWE KWA SABABU YA YALE YALIYO TANGULIZWA NA MIKONO YAO; NA ALLAH NI MWENYE KUWAJUA VYEMA WANAO DHULUMU. NA HAKIKA UTAWAONA NI WENYE KUWASHINDA WATU WOTE KWA PUPA YA KUISHI, NA KULIKO WASHIRIKINA. KILA MMOJA WAO ANATAMANI LAU ANGELI PEWA UMRI WA MIAKA ALFU. WALA HAYO YA KUZIDISHIWA UMRI HAYAMUONDOSHEI ADHABU; NA ALLAH ANAYAONA WANAYO YATENDA”. [02:94-96]

 Endelea ...


 

Nyakati za Swala
Tafsiri ya Qur-an

Aya ya Wiki

JE! HAWATEMBEI KATIKA ARDHI ILI WAPATE KUWA NA NYOYO ZAO ZA KUZINGATIA, AU MASIKIO YA KUSIKILIA? KWANI HAKIKA SI MACHO YANAYO POFUKA, LAKINI ZINAZO POFUKA NI NYOYO ZILIOMO VIFUANI”. [22:46]


Hadith ya Wiki

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Muumini hakupata faida baada ya kumcha Allah, na kitu kilicho bora kuliko (kumpata) mke mwema, akimuamrisha humtii, akimtazama humfurahisha. Akimuapia hukitakasa kiapo chake na akighibu (akiwa mbali) nae, humuhifadhia nafsi yake na mali yake”. Ibn Maajah-Allah amrehemu. 


Katazo la Wiki

Mtumishi/mfanya kazi wako ni mtu kamili kama ulivyo wewe, ila tu ni kwamba Allah kwa hekima na mapenzi yake amemuweka chini yako, ili mtegemeane kimaisha. Sasa kwa nini unajikweza juu yake, unamdharau, unamnyanyasa na pengine hata kumpiga?! Ikiwa Bwana Mtume, naye ndiye bora wa viumbe hakufanya hivyo, wewe nani hata uyafanye hayo?! Msikilize mtumishi bora Anas bin Maalik anavyo msifia Bwana bora: “Nilimtumikia Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-kwa kipindi cha miaka ishirini, wallah hakupata kuniambia katu ah! Wala hakupata kusema kwa nini umefanya hivi au kwa nini hukufanya kadha”. Muslim-Allah amrehemu.

 

Swali la Wiki

SWALI: Nini hukumu ya mwanamke kumuingilia mkewe naye akiwa hedhini?

JIBU: Mwanamume kumuingilia mkewe katika hali ya hedhi, ni jambo lililo harimishwa kwa nassi (nukuu) ya Qur-ani na Sunna. Allah Ataadhamiaye anasema: “NA WANAKUULIZA JUU YA HEDHI. WAAMBIE, HUO NI UCHAFU. BASI JITENGENI NA WANAWAKE WAKATI WA HEDHI. WALA MSIWAINGILIE MPAKA WATWAHIRIKE...”. [02:222]

Mwanamume atakapo thubutu kumuingilia mkewe ndani ya kipindi cha hedhi, kumemlazimu kuleta toba na kutokurudia tena kitendo hicho na pia amewajibikiwa na kafara, nayo ni kutoa dinari moja au nusu ya dinari. Hilo ni kwa mujibu wa hadithi ya Ibn Abbas-Allah amuwiye radhi-katika kadhia ya yule aliye muingilia mkewe naye akiwa hedhini, alisema: “Atoe sadaka ya dinari moja au nusu dinari”. Ahmad, Abu Daawoud, Tirmidhiy & Nasaai-Allah awarehemu.

Na muradi wa “dinari” ni tola (mithqaali) moja ya dhahabu, akitoipata basi inatosha thamani yake katika fedha.

Allah ndiye Mjuzi mno.



| Tuandikie |



: