Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao !!!

 

Akhlaaq-Tabia  

"Hakika si vingine nimetumwa kuja kutimiza TABIA NJEMA" Hadith Tukufu

FADHILA/UBORA WA SUNNA CHINI YA KIVULI CHA SUNNAH

 Faida

 

         ii.          Fadhila/ubora wa subira chini ya kivuli cha Sunnah (hadithi):

              Na miongoni mwa yaliyo pokewa katika Sunnah katika kutaja fadhila/ubora wa subira, ni hadithi zifuatazo:

1.      Imepokewa kutoka kwa Anas-Allah amuwiye radhi-kwamba Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Hakika Allah Ataadhamiaye amesema: Nitakapo muonja mja wangu kwa vipenzi vyake viwili [macho], kisha akasubiri, nitampa badali ya pepo kutokana na viwili hivyo”. Bukhaariy [10/100]-Allah amrehemu.

2.      Imepokewa  kutoka kwa Abu Hurayrah-Allah–amuwiye radhi-kwamba Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Allah amesema: Hana mja wangu muumini kwangu mimi malipo yoyote pindi nitakapo ichukua roho ya mpenzi wake miongoni mwa watu wa dunia, ila pepo”. Bukhaariy [11/207]-Allah amrehemu.

3.      Imepokewa kutoka kwa Atwaa Ibn  Abi Ribaah amesema: Ibn Abbas-Allah amuwiye radhi-aliniambia: Je, nisikuonyeshe mwanamke  katika watu wa peponi? Nikamjibu: Kwani [nionyeshe]. Akasema: Huyu mwanamke mweusi [umuonaye], alimjia Mtume-Rehema na Amani zimshukie-akasema: Hakika mimi ninaangushwa na kifafa na ninafunukwa na nguo, basi niombee kwa Mungu (aniponye). Mtume akasema: “Ukitaka subiri na utapata pepo na ukitaka nitakuombea Mungu akuafu”. Akasema: Nitasubiri, kisha akasema: Hakika mimi ninafunukwa na nguo [nikiangushwa), basi niombee kwa Mungu nisifunukwe. Mtume akamuombea”. Bukhaariy [10/99] & Muslim [2576]-Allah awarehemu.

4.      Imepokewa kutoka kwa Abu Saidi Al-Khudriy-Allah amuwiye radhi-kwamba Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie- amesema: “...na atakaye isubirisha nafsi yake, Allah atampa nguvu za kusubiri. Na hakupata kupewa mtu kipawa bora na kikunjufu kuliko subira”. Bukhaariy [11/303] & Muslim [1053]-Allah awarehemu

5.      Imepokewa kutoka kwa Swuhaibu Ar-ruumiy-Allah amuwiye radhi-amesema: Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Ajabu iliyoje kwa jambo la muumini, hakika jambo lake lote ni kheri na hilo haliko kwa yeyote ila kwa muumini. Ikimfika raha hushukuru, basi ikawa ni kheri kwake na ikimfika dhara [taabu], husubiri na ikawa ni kheri kwake”. Muslim [2999]-Allah amrehemu.

6.      Imepokewa kutoka kwa Jaabir-Allah amuwiye radhi-amesema: Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-alisema: “Watatamani watu wenye afya [duniani] siku ya Kiyama, pale watu walio onjwa [kwa maradhi hapa duniani] watakapo pewa thawabu. Lau kwamba ngozi zao zingekatwa kwa mikasi”. Tirmidhiy [2402]-Allah amrehemu.

7.      Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah-Allah amuwiye radhi-amesema: Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Mabalaa hayaachi kumuandama muumini mwanaume na muumini mwanamke, katika nafsi yake, watoto wake na mali yake, mpaka akutane na Allah ilhali hapana dhambi yoyote juu yake”. Tirmidhiy [2399] & Al-Haakim [4/314]-Allah awarehemu.

8.      Imepokewa kutoka kwa Ummu Salamah-Allah amuwiye radhi-amesema: Nilimsikia Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-akisema: “Hapana muislamu yeyote anaye patwa na msiba akasema aliyo amrishwa na Allah [kuyasema wakati huo]: “INNAA LILLAAHI WA INNAA ILAYHI RAAJIUUN-HAKIKA SISI NI WA ALLAH, NA KWAKE YEYE HAKIKA TUTAREJEA”...Ewe Mola wa haki! Nakuomba unipe ujira  katika  msiba huu na unipe badali bora kuliko huo [msiba] akisema hivyo, Ila Allah atampa badali bora kuliko huo. (Anaendelea) kusema: Zama alipo kufa Abu Salamah [mume wangu], nikasema: Nani [mume] bora kuliko Abu Salamah; swahaba wa Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie? Halafu Allah akanitia azma, basi nikasema [maneno] hayo [aliyo yafundisha Allah]. Anasema: Basi nikaolewa na Mtume wa Allah”. Muslim [918]-Allah amrehemu.

9.      Imepokewa kutoka kwa Abu Maalik Al-Ashiariy-Allah amuwiye radhi-amesema: Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Twahara ni sehemu ya imani na AL-HAMDULILLAH inajaza mizani [ya mja siku ya hisabu]. NA SUB-HAANALLAH na AL-HAMDULILLAH zinajaza (thawabu zake eneo) lililo baina ya mbingu na ardhi. Na swala ni nuru, sadaka ni hoja, subira ni mwangaza na Qur-ani ni hoja ya kukuokoa [ukiifuata] au kukuangamiza [ukiacha kuifuata]. Watu wote hudamka, basi mwenye kuiuza nafsi yake, yuko mwenye kuikomboa [na moto] au mwenye kuiangamiza”. Muslim [234]-Allah amrehemu.

 

Ndugu mwema-Allah akurehemu-huu ni mpetwapetwa tu ulio chujwa kutoka katika mlango wa kutaja fadhila/ubora wa subira. Na lau si kuchelea urefusho wenye kuchosha, basi tungeendelea kukuletea utungo wa fadhila hizo chini ya kivuli cha maneno ya Mtume wako-Rehema na Amani zimshukie. Na tunataraji katika hadithi chache hizi tulizo zinukuu, kuna mazingatio na ukumbusho: “...KWA MWENYE MOYO AU AKATEGA SIKIO...” [50:37] Kama ambavyo kuna ndani yake kani impelekeayo mja mwema kusubiri katika yote yanayo msibu huku akiamini kuwa: “HAUTOKEI MSIBA KATIKA ARDHI WALA KATIKA NAFSI ZENU ILA UMEKWISHA ANDIKWA KATIKA KITABU KABLA HATUJAUUMBA...” [57:22]

 

  



 | Tuandikie |