|
Suna za
Posa:
Kunasuniwa kwa mposaji au wakili wake, kutanguliza khutuba kabla ya kuleta tamko
la posa na kabla ya kifungo cha ndoa. Aianze hiyo khutba kwa kumuhimidi Allah na
kisha kumswalia Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie. Hayo ni kwa mujibu wa
hadithi isemayo: “Kila jambo jema lisilo anzwa kwa kumuhimidi Allah, basi
jambo hilo ni lenye kukatika (baraka)”. Ibn Maajah [1894]-Allah amrehemu.
Baada ya kumuhimidi Allah, ausie kumcha Allah, halafu ndipo ayadhihirishe
matashi yake kwa kusema: Nimekujilieni kumposa binti yenu.
Pia kunasuniwa
kwa walii wa mposwaji (binti/mwanamke), nae kukhutubu na kusema baada ya
kumuhimidi Allah, kumswalia Mtume na kuusia kumchaMngu: Wewe si mwenye
kukataliwa.
Na khutba
itolewayo kabla ya kufungwa kwa ndoa, imekokotezwa mno kuliko ile khutba
itolewayo kabla ya posa. Kwa sababu ya kupokelewa hilo kwa Salafu wema-Allah
awawiye radhi.
Maimamu-Allah
awawiye radhi-wametabaruku kwa yaliyo pokewa kutoka kwa Ibn Masoud-Allah amuwiye
radhi-amesema: “Atakapo taka mmoja wenu kukhutubu kwa haja ya ndoa au jambo
jinginelo, basi na aseme: INNAL-HAMDA LILLAAH, NAHMADUHU WANASTA’INUUHU
WANASTAGHFIR-HU. WANAUDHU BILLAAHI MIN SHURUURI ANFUSINAA WASAYYIAATI
A’AMAALINAA. MAN YAHDIHIL-LAAHU FALAA MUDHWILLA LAHU, WAMAN YUDHWLIL FALAA
HAADIYA LAHUU. WA ASH-HADU AN LAA ILAAHA ILLAL-LAAHU WAHDAHU LAA SHARIYKA LAHUU.
WA ASH-HADU ANNA MUHAMMADAN ABDUHU WA RASUULUH. {YAA AYYUHAL-LADHIYNA
AAMANUT-TAQUL-LAAH HAQQA TUQAATIHI WALAA TAMUUTUNNA ILLA WA ANTUMUM-MUSLIMUUN}.
{YAA AYYUHAN-NAASUT-TAQUU RABBAKUMUL-LADHIY KHALAQAKUM-MIN NAFSIN WAAHIDAH, WA
KHALAQA MIN-HAA ZAUJAHAA WA BATTHA MIN-HUMAA RIJAALAN KATHIYRAA WA NISAA.
WAT-TAQUL-LAAHAL-LADHIY TASAALUUNA BIHII WAL-ARHAAM, INNALLAAH KAANA ALAYKUM
RAQIYBA}. {YAA AYYUHAL-LADHIYNA AAMANUT-TAQUL-LAAH WAQUULUU QAULAN SADIYDAN.
YUSWLIH LAKUM A’AMAALAKUM WAYAGHFIR LAKUM DHUNUUBAKUM. WAMAN YUTWI’IL-LAAH WA
RASUULIHI FAQAD FAAZA FAUZAN ADHWIYMA}.
Tafsiri ya
khutuba:
“Hakika himidi
zote njema ni zake Allah, tunamuhimidi Yeye, tunamuomba msaada na tunamtaka
maghufira Yeye. Na tunajilinda kwa Allah kutokana na shari ya nafsi zetu na
matendo yetu maovu (mabaya). Aongolewaye na Allah, basi hapana wa kumpoteza. Na
ampotezaye, basi hapana wa kumuongoa.
Na ninashuhudia
kwamba hapana Mola afaaye kuabudiwa kwa haki ila Allah peke yaka, hana mshirika.
Na ninashuhudia kwamba Muhammad ni mja na mjumbe wake.
“ENYI MLIOA
AMINI! MCHENI ALLAH KAMA IPASAVYO KUMCHA; WALA MSIFE ILA NANYI NI WAISLAMU”.
[03:102]
“ENYI WATU!
MCHENI MOLA WENU MLEZI ALIYE KUUMBENI KUTOKANA NA NAFSI MOJA, NA AKAMUUMBA MKEWE
KUTOKA NAFSI ILE ILE. NA AKAENEZA KUTOKANA NA WAWILI HAO WANAUME NA WANAWAKE
WENGI. NA TAHADHARINI NA ALLAH AMBAYE KWAYE MNAOMBANA, NA JAMAA ZENU. HAKIKA
ALLAH NI MWENYE KUWAANGALIENI”. [04:01]
“ENYI MLIO
AMINI! MCHENI ALLAH NA SEMENI MANENO YA SAWA SAWA. APATE KUKUTENGENEZEENI
VITENDO VYENU NA AKUSAMEHENI MADHAMBI YENU. NA ANAYE MT’II ALLAH NA MTUME WAKE,
BILA YA SHAKA AMEFANIKIWA MAFANIKIO MAKUBWA”. [33:70-71]
Hukumu ya
wachumba kukaa faragha na kuchanganyika pamoja kabla ya ndoa:
Ni
jambo lililo tangaa na kuenea katika baadhi ya familia za Kiislamu, familia
zilizo mbali na uelewa wa Uislamu katika wigo wa ndoa. Kwamba mposaji akisha
leta posa tu, tayari anakuwa huru kukaa faragha, kuchanganyika na hata kuwa na
matembezi ya pamoja na mchumba wake. Haya yanafanyika chini ya mwavuli wa kile
kinacho itwa “kuzoena na kufahamiana kitabia”. Zoezi hili linafanyika kwa kila
mmoja wao kujitahidi kujivika na kujipamba sifa/tabia ambazo si za uhalisia
wake, ili tu kumuonyesha mwenzake kuwa yeye ndiye chaguo lake halisi, sahihi na
stahiki.
Kwa janibu ya
sharia inayo randana sawa na maumbile ya mwanaadamu, hakika kadhia ya wachumba
kuchanganyika na kukaa faragha pamoja. Ni jambo lililo harimishwa na wala si tu
haliridhiwi na Allah na Mtume wake, bali hata na akili ya kawaida tu. Katika
hili Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-anatuongoza kwa kusema:
“Mwanaume asikae faraghani na mwanamke ila awe pamoja nao maharimu”.
Bukhaariy [4935] & Muslim [1341]-Allah awarehemu.
Chini ya
mwangaza wa sharia ya Kiislamu, binti/mwanamke mchumbiwa/mposwaji kabla ya
kufungwa kwa ndoa, huzingatiwa kama mwanamke ajinabiya na hivyo kuchukua hukumu
zake zote.
Ama baada ya
kufungwa na kusihi kwa kifungo cha ndoa, hapo tena faragha na mchanganyiko
umesha halalika. Kwa sababu binti/mwanamke huyo amekiwsha kuwa mke wake aliye na
uhuru nae kama ule ambao yeye mke anao kwake yeye mume.
|