|
Ulazimu wa
waq-fu na hukumu zinazo uandamia:
Waq-fu ni
miongoni mwa vifungu lazimishi ambavyo vinavyo andamiwa na athari zake (vifungo
hivyo), mara tu kinapo anzishwa (fungwa) kifungo kilicho sahihi. Na waq-fu si
kama wasiya, kwani huo (wasiya) ni kifungo juzishi.
Ulazimu wa
kifungo cha waq-fu unaandamiwa na hukumu zifuatazo:
-
Kutokuthibiti kwa khiari katika kifungo cha waq-fu. Angalia, mtu atakapo
funga waq-fu ulio sahihi katika sheria, hatakuwa na khiyari majlisi kama
ambavyo pia asivyo kuwa na khiyari sharti.
- Uguro
(uhamaji) wa umiliki wa chenye kuwekwa waq-fu kutoka kwa muweka waq-fu
kwenda kwa Allah Ataadhamiaye. Kwa hivyo basi, mmiliki wa asili (mwanzo)
hana haki ya kuusarifu waq-fu alio utoa kwa njia ya umiliki, si kwa kuuza au
kwa kutoa hiba, wala kwa namna nyingineyo.
- Uguro wa
haki ya kunufaika na waq-fu kwenda kwenye jiha (upande) ambao ulio wekewa
waq-fu huo, ukiwa ni makhsusi (upande huo) au ni wa umma (wa watu wote).
Umiliki wa
chenye kuwekwa waq-fu:
Muweka
waq-fu atakapo weka waq-fu kitu dhati (kilicho thibiti mahala pake) au mali
hamishika. Au akaweka waq-fu silaha, gari au kitu kinginecho. Milki ya chenye
kuwekwa waq-fu itaguria (itahamia) kwa Allah Ataadhamiaye, kwa hivyo basi
kilicho wekwa waq-fu hakitakuwa tena ni milki ya muweka waq-fu, wala milki ya
muwekewa waq-fu (mnufaika wa waq-fu).
Manufaa ya
chenye kuwekwa waq-fu:
Manufaa ya kitu dhati kilicho wekwa waq-fu, ni milki ya yule aliye wekewa/pewa
waq-fu huo, akiwa ni muainiwa. Na kunamuelea kuyatwaa manufaa hayo yeye mwenyewe
moja kwa moja, mfano wa nyumba akaishi humo. Au akayatwaa kwa kupitia kwa mtu
mwingine, kwa njia ya kuazimisha au kukodisha.
Pia anamiliki
faida za waq-fu huo zinazo patikana baadaye, kama vile matunda ya miti iliyo
wekwa waq-fu. Na sufi na maziwa ya watoto wa wanyama walio wekwa waq-fu.
Ama pale
muweka/mpewa waq-fu atakapo kuwa si muainiwa (hakutajwa), akawa ni pande
miongoni mwa pande kama vile mafakiri. Hakika wao hawamiliki manufaa ya chenye
kuwekwa waq-fu, bali wanamiliki haki ya kunufaika nacho.
Haki/mamlaka
ya kutumia kilicho wekwa waq-fu:
Hakujuzu kuwa na haki/mamlaka ya kutumia dhati ya kilicho wekwa waq-fu, si kwa
kuuza au kununua, si kwa kutoa hiba au kurithi. Yote hayo hayajuzu si kwa upande
wa muweka waq-fu tu bali hata kwa mpewa waq-fu muainiwa au asiye muainiwa. Bali
dhati ya kitu hicho inaendelea kubakia chini ya umiliki wa Allah Ataadhamiaye,
manufaa yake yakitolewa kwa wale walio wekewa waq-fu huo. Na utumike kadiri
imkinikavyo kwa mujibu wa maelezo ya muweka waq-fu.
Hilo
linafahamishwa kupitia waq-fu wa Sayyidna Umar bin Al-Khatwaab-Allah amuwiye
radhi-kwani yeye alitoa maelezo katika waq-fu wake: “Ya kwamba hauuzwi,
hautolewi hiba na wala haurithiwi”. Bukhaariy [2586] & Muslim [1632]-Allah
awarehemu.
Masurufu ya
kilicho wekwa waq-fu:
Ikiwa
chenye kuwekwa waq-fu kinahitajia masurufu (gharama za kujikimu), kama vile
chakula cha wanyama (wawekwa waq-fu), au ukarabati wa majengo, au utengenezaji
wa ala/zana. Hakika gharama hizo juu ya waq-fu, zitakuwa kwa namna aliyo
ishurutizia muweka waq-fu kutoka katika mali yake mwenyewe au kutoka kwenye mali
ya waq-fu wenyewe. Kama muweka waq-fu hakuweka sharti lolote, gharama zitatoka
kwenye mazao/mapato ya waq-fu ikiwa unayo mazao/mapato. Angalia, iwapo
kiwekwacho waq-fu hakina mazao/mapato au manufaa yake yalisita (simama). Hapo
katika hali/mazingira hayo, gharama zitaiwajibikia Baytul-Maali ya Waislamu, kwa
sababu ndio inayo husika na maslahi yao. Na katika utoaji wa gharama za kiwekwa
waq-fu, kuna maslahi kwao (hao Waislamu).
Kuhiliki/kuangamia kwa kiwekwa waq-fu na hukumu zinazo fungamana nako:
Kiwekwa waq-fu kinaweza kuhiliki, basi kwa sababu ya kuhiliki huko zinatungamana
hukumu kadhaa wakati huo. Hukumu zinazo tofautiana kufuatia utofauti wa kitu
dhati kilicho wekwa waq-fu, kilicho hiliki na kwa utofauti wa aina ya hilaki. Na
hukumu hizo ni kama zifuatavyo:
- Iwapo
kiwekwa waq-fu ni mnyama asiye liwa, akafa, atahusishwa na ngozi yake yule
aliye wekewa/pewa waq-fu huo, kwani yeye ndiye mstahiki zaidi wa kupewa
kuliko mwenginewe. Angalia, ngozi hiyo ikisafishwa na kuwa mali ghafi
(dabghu), itarejea kuwa ni waq-fu juu yake, atanufaika nao. Na wala
hakumjuzii kuiuza ili kuendelea kuhifadhi makusudio ya muweka waq-fu, kwa
kadiri itakavyo mkinika.
- Iwapo
kiwekwa waq-fu ni mnyama aliwaye, na muwekewa waq-fu akakata shauri ya
kwamba mnyama huyo atakufa kutokana na janga lililo mpata. Hapo kunajuzu
kumchinja kwa sababu ya dharura hiyo na nyama yake itauzwa na kwa thamani
yake atanunuliwa mnyama mwingine kama huyo na atawekwa waq-fu mahala pake.
Na pamesemwa suala la nyama yake litaachwa mikononi mwa hakimu/mtawala,
afanye kwa nyama hiyo lile analo ona lina maslahi.
- Kitakapo
tilifiwa kitu dhati kilicho wekwa waq-fu, ikiwa hivyo basi ni juu ya mtilifu
wake kulipa kima/thamani yake. Hilo litakuwa kama vile mtu atakapo kitilifu
kwa makusudi. Muwekewa waq-fu hatomiliki kima cha kitu dhati kilicho wekwa
waq-fu ambacho kimetilifiwa, lakini kitanunuliwa kitu dhati kinacho fanana
na kile kilicho tilifiwa, kwa kima hicho. Na kitu dhati hicho kitakuwa
waq-fu mahala pa kile kilicho tilifiwa. Na hilo linafanyika ili kuchunga
lengo la muweka waq-fu, yaani ule uendelevu wa thawabu. Na ili kufungamana
haki ya tumbo la pili na la baada yake na kitu dhati hicho. Angalia,
ikishindikana kununua kitu dhati kamili, basi na kinunuliwe baadhi ya kitu
dhati hicho, kwa sababu hicho ndicho kilicho karibu mno na makusudio ya
muweka waq-fu. Ama kitakapo tilifu hicho kitu dhati kilicho wekwa waq-fu
bila ya kuwa na dhamana, au kilitilifika chenyewe, hapo waq-fu (thawabu)
utakuwa umekoma kwa sababu ya kuondoka dhati ya kitu kilicho wekwa waq-fu.
- Yatakapo
fungika manufaa ya kitu dhati kilicho wekwa waq-fu kwa sababu isiyo na
dhamana, kama vile mtu kuweka waq-fu miti, kisha ikakauka au ikang’olewa na
upepo au mumbwi. Na isiwezekane kuirejesha mahala pa upando wake kabla ya
kukauka, (thawabu za) waq-fu haujakatika, bali itaendelea kuwa katika hukumu
ya waq-fu. Yakipatiwa manufaa mashina yake kwa kukodishwa na kwa namna kama
hiyo, ili kuudumisha waq-fu katika dhati yake. Wala miti hiyo haitauzwa wala
kutolewa hiba. Angalia, iwapo kunufaika nayo (miti hiyo) hakutapatikana ila
kwa njia ya kuimaliza kabisa, kwa kuichoma (mkaa) na mfano wake, kunamjuzia
muwekewa waq-fu kufanya hivyo. Ila tu ni kwamba hakujuzu kuiuza wala kuitoa
hiba.
- Kitakapo
kuwa kiwekwa waq-fu ni majamvi/mikeka/mabusati ya msikiti, yakalowa maji. Au
kitakapo kuwa ni mashina, yakakatika na yasifae ila kwa kuunguzwa moto. Hapo
kumejuzu kuyauza ili yasipotee bure au yasijaze nafasi pasina faida yoyote.
Na kupata mali kidogo kutokana na thamani yake, itakayo rudi kwenye waq-fu,
ni bora kuliko kupotea bure. Na kwa msingi huu basi, hakika thamani yake
itatumiwa katika maslahi ya msikiti. Na katika maslahi hayo, utatangulizwa
ununuzi wa mfano badala wa kile kilicho tilifu, limkinikapo hilo.
Ama yatakapo faa kwa matumizi yasiyo kuunguza moto, hapo
hakujuzu kuyauza, ili kuhifadhi kubakia dhati yake, ili kwenda sanjari na lengo
la muweka waq-fu.
- Msikiti
utakapo bomoka na kukashindikana kuujenga upya, hakujuzu kuuza (kiwanja) kwa
hali yoyote ile, kwa sababu ya kuwepo imkani ya kuweza kuujenga tena wakati
wowote. Angalia, iwapo msikiti huo unayo mapato yanayo tumika kwa maslahi
yake, tukitarajia kuujenga upya, basi kunajuzu kuyatumia mapato hayo kwenye
maslahi ya msikiti ulio jirani na hapo.
- Msikiti
utakapo hofiwa kukumbwa na janga lolote, kunamjuzia hakimu/mtawala kuutengua
na akayatumia mawe/matofali yake kujengea msikiti mwingine. Na wala
mawe/matofali na kifusi chake kisijengewe kitu kingine, kwa ajili ya
kulichunga lengo la muweka waq-fu. Na kuujenga huo (msikiti upya) karibu na
ule msikiti ulio tenguliwa, ni bora zaidi.
- Lau mtu
ataweka waq-fu mali kwa ajili ya ujenzi wa daraja kwenye korongo kavu la
mto, korongo hilo likameguka na kupelekea daraja kubomoka. Na watu
wakahitajia daraja jengine, hapo kunajuzu kulihamisha daraja hilo kulipeleka
mahala linapo hitajika, ili kuyabakisha madhumuni ya muweka waq-fu kwa
kadiri ya imkani.
|