|
Sharti
tunazozikusudia hapa ni zile sharti za kusihi swala.
Maana
ya sharti :-
Sharti
ya kitu ni lile jambo au tendo ambalo upatikanaji wa kitu husika
unalitegemea jambo/tendo hilo lakini lenyewe si sehemu ya kitu hicho.
Mfano
: wa ufafanuzi
Mmea ili upatikane/uwepo
juu ya uso wa ardhi unahitaji mvua pamoja na ukweli kwamba mvua sio sehemu
ya mmea huo. Kwa hivyo basi
mvua ni sharti katika upatikanaji na kuwepo kwa mmea kwani bila ya mvua
hakuna mmea lakini bado mvua haiwi ni sehemu ya mmea huo.
Baada
ya kujua ainisho la sharti, hebu sasa tuziangalie sharti za kusihi kwa
swala moja baada ya jingine kwa ufafanuzi wa kina sharti za kusihi swala
ni nne zifuatazo:-
1.
TWAHARA:-
Hii
ndio sharti ya kwanza ya kusihi swala:
Twahara nni nini, tayari umekwishajifunza katika sura ya kwanza,
somo la kwanza, rejea huko na utaona. Twahara ambayo ni sharti ya kusihi
swala imegawanyika katika matapo yafuatayo:-
(i)
Twahara ya mwili kutokana na hadathi .
mtu mwenye hadathi haisihi swala yake.
Ni mamoja ikiwa ni hadathi ndogo ambayo ni ukosefu wa udhu au ni
hadathi kubwa kama vile janaba. Haya
ni kwa mujibu wa kauli ya Mtume – Rehema na Amani zimshukie katika
hadithi sahihi “Haikubaliiwi swala bila ya twahara – Muslim.
(ii)
Twahara ya mwili kutokana na najisi.
Rejea sura ya kwanza, somo la pili ili ujikumbushe maana ya najisi
na aina zake. Kabla ya
kuvaana na ibada ya swala ni lazima mtu ahakikishe kuwa mwili wake ni
twahara, hauna najisi ya aina yoyote ile.
Haya ndio tunayoyafahamu kutokana na kauli ya Bwana Mtume –
rehema na Amani zimshukie: “Jiepusheni na mkojo kwani hakika sehemu kubwa ya adhabu (zimpatazo
mja) kaburini ni kwa sababu ya kutojikinga nao”
Mkojo
hapa unakuwa ndio kigezo na mfano wa najisi nyingine zote ambazo Mtume
hakuzitaja hapa katika hadithi hii. Bwana mtume Rehema na Amani zimshukie – alimwambia
Bi. Fatmah Bint Abiy Hubaysh – Allah amuwiye radhi;
:Itakapokuja hedhi basi acha kuswali.
Ikikoma, basi jikoshe damu (jitwaharishe na uanze) kuswali”
Bukhaariy na Muslim.
iii.
Twahara ya nguo
kutokana na najisi. Haitoshi
tu mwili kuwa na twahara usio na najisi
bali hapana budi nguo anazozivaa mwenye kutoka kuswali, pia ziwe ni
twahara, zisiwe na najisi ya aina yoyote ile.
Hivyo ndivyo tunavyoambiwa na Mwenyezi mungu Mtukufu kupitia kauli
yake : NA NGUO ZAKO
UZITWAHARISHE (74:4) Haisihi
swala ya mtu aliyeswali huku akiwa kavaa nguo yenye najisi isiyosameheka
kisheria hata kama mwili wake utakuwa ni twahara.
Imepokelewa kutoka kwa Abu- Hurayrah – Allah amuwiye radhi –
Kwamba Bi., Khaulah Bint Yassar – Allah amuwiye radhi alimuendea Mtume
na kumwambia : Ewe Mtume wa
Allah mimi sina ila nguo moja
tu, nami ninapata hedhi katika nguo hiyo, basi nifanyeje?
(Mtume) akamwambia “Utakapotwaharika ifue (itwaharishe) (pia) na
iswalie |” Akauliza (tena) Kama (athari ya) damu haikutoka?
(Mtume) akamjibu “ Kunakutosha kukosa damu, na wala athari ya
damu haikudhuru : Abuu Dawood.
d.
Twahara ya mahala pa kuswalia.
Ni lazima kwa mwenye kutaka kuswali ahakikishe
mahala anapotaka kupatumia kwa ajili ya utekelezaji wa ibada yake
hiyo ya swala ni twahara,
hapana najisi yoyote ile. Sharti
hili tunaliegemeza katika riwaya iliyopokelewa na Abu Hurayrah – Allah
amuwiye radhi amesema Alisimama
mkazi mmoja wa majangwani akakojoa msikitini (msikiti wa Mtume) watu (mwaswahaba)
wakamuinukia ili wamtie adabu. Mtume
– rehema na Amani zimshukie akawaambia
“
Muacheni (amaliza haja zake) na (kisha) mumwagie mkojo wake ndoo ya maji,
kwani hakika si vinginevyo mmetumizwa kuwa wawepesishaji (wa mambo) na
wala hamkutumwa kuwa wafanya uzito/ugumu – Bukhaariy.
2.
ELIMU/MAARIFA YA KUINGIA WAKATI WA SWALA
Hii
ndio sharti ya pili ya kusihi kwa swala umekwishajua kutokana na maelezo
ya darasa zilizotangulia kwamba kila swala ya fardhi ina wakati wake
maalum. Ili swala
yako isihi ni lazima uiswali ndani ya wakati huo.
Haitoshi tu kuwa swala inaswaliwa ndani ya wakati kwa sadfa au
kubahatisha. Bali ni lazima
mwenye kutaka kuvaana na swala aijue wakati kupitia elimu/maarifa.
Hii ni kwa sababu ya kutokusihi kwa swala
ya mwenye kuswali bila ya kujua kuingia itambarikiwa baada ya
kumaliza kuswali kuwa amesadifu wakati Mwenyezi Mungu Mtukufu anatuambia
………………… kwa HAKIKA SWALA KWA WAUMINI NI FARDHI ILIYOWEKEWA
NYAKATI MAKHSUSI 4:103.
NAMNA
YA KUJUA KUINGIA WAKATI WA SWALA
NI
vipi basi tunaweza kutambua kuwa wakati wa swala fulani umeingia ?
Hili litawezakana kwa kutumia mojawapo ya njia tatu
zifuatazo:-
1.
maarifa yakinifu:
Mtu
atumie dalili hisia (zinazofahamika kupitia milango ya fahamu) kama vile
kuliona jua likizama baharini (upande wa bahari)
2.
Jitihada binafsi
Mtu
anaweza kutegemea dalili dhahania hizi ni dalili zisizo za moja kwa moja.
Dalili hizi ni pamoja na kivuli, kipimo cha kazi fulani yaani muda
inaochukua kazi hyo. Mtu
anaweza kusema mathalan kwa kawaida nikianza kushona suruali baada ya
adhuhuri mpaka nimaliza huwa ni alasiri tayari.
3.
Kufuata Mjuzi
Itakaposadifu
kwamba mtu hana maarifa yakinifu wala hawezi kufanya jitihada binafsi.
Huyu ni yule mtu
ambaye hazijui nyakati za swala zinaingia saa ngapi na hana maarifa ya
kutumia dalili hisia wala dhania kumsaidia kujua wakati wa swala.
Yeye huyu ina ataamua kumfuata mtu mjuzi mwenye maarifa ua kuingia
na kutoka kwa, nyakati za swala kwa kutegemea dalili hisia.
Akimwambia wakati bado haujaingia basi na asubiri au, atamfuata mtu
mwenye kutumia jitihada binafsi kwa kutegemea dalili dhania.
FAIDA:
HUKUMU YA SWALA ILIYOSWALIWA NJE YA WAKATI.
Tunaposema
swala iliyoswaliwa nje ya wakati hatumaanishi zaidi ya ile swala
iliyosaliwa kabla ya kuingia wakati wake.
Ni vipi basi hukumu ya swala hii?
Kwa msaada wa Mwenyezi Mungu tunasema na il-hali
Yeye ndiye Mjuzi mno. Itakapombainikia
mtu kwamba swala aliyoiswali; ameiswali nje ya wakati, yaani kabla ya kuingia wakati wake.
Kisheria swala hiyo itazingatiwa
kuwa ni BATILI na
ITAMUWAJIBIKIA kuiswali tena ndani ya wakati, bila ya kujali kuwa akiswali
kwa kutegemea.
·
Maarifa yakinifu
·
Jitihada binafsi au kwa
·
Kumfuata mjuzi
Swala
itakuwa ni batili kwa sababu ya kukosekana sharti mojawapo ya kusihi swala.
3.
KUSITIRI UTUPU-UCHI
Hii
ndio sharti ya tatu miongozi mwa zile sharti nne za kusihi kwa suala.
Ili tuweze kuijua vema
sharti hii hatuna budi kwanza tuyajue
mambo yafuatayo:
i)
maana ya utupu
Kisheria
utupu ni kila ile sehemu ya mwili ambayo ni wajibu lkuisitiri au ni haramu
kuiangalia/kwaangaliwa
ii)
Mipaka ya utupu ndani ya swala, ndani ya swala ni lile aneo lote
lililo baina ya kitovu na magoti yake.
Ni wajibu eneo lote hili lisitiriwe .
Mwenyezi MUNGU anasema
“ENYI WANAADAMU CHUKUENI MAPAMBO YENU WAKATI WA KILA SWALA”
(7.32)
Muradi
wa neno Mapambo ni nguo inayositiri utupu.
Hivi ndivyo ilivyotasfririwa na wataalamu wa fani ya tafsiri.
Fahamisho la aya ni kuwa Enyi wanadamu sitirini tupu zenu mnapotaka
kuswali. Imepokelewa hadithi
na Said – Al-Khudriy – Allah amuwiye radhi kwamba mtume Rehema na
Amani zimshukie amesema “
Utupu na mwaname ni baina ya kitovu chake mpaka gotini kwake.
(iii)
Kwa upande wa mwanamke
: Ni mwili wake wote
ukiondoa uso na vitanga vya mikono; Sehemu yote hiyo ya mwili ni
wajibu isitiriwe. Hivyo
ndivyo tunavyoelewa kupitia kauli ya Mwenyezi Mungu … wala
wasidhihirishe viungo vyao isipokuwa VINAVYODHIHIRIKA
Jamhuri
ya Mafaqihi
wamesema kuwa muradi wa kauli “vinavyodhihirika” ni uso na vitanga
-
Imeshurutizwa nguo ya kujisitiri-
-
Isiwe
nyeupe sana kiasi cha kuonyesha rangi
ya mwili mpaka
Mtazamaji
akatambua weupe ua weusi wa
mwili.
-
Isiwe
inabana kiasi cha kiliacha finyango la mwili lidhihirike.
Inapendeza kwa muumini kuitekeleza ibada
ya swala akiwa katika mavazi twahara , nadhifu,
mazuri ayapendayo , akiyavaa roho yake hutua
na kuburudika. Tunasema hivi kwa sababu
nguo inaweza kuwa twahara lakini sio nadhifu
wala nzuri
C/.
Mipaka ya utupu nje ya swala
i/.
Mwanamume mbele ya mwanamume wenziwe na wanawake walio maharimu zake ni
sehemu ya mwili iliyo baina kitovu na magoti.
Ama
mbele ya wanawake “ajnabiyyat” wa kando na kando wasio
maharimu ni mwili wake wote
isipokuwa na vitanga kauli
yenye kutegemewa katika riwaya ya Ummu Salamah –Allah aminiye radhi –asema
Nilikuwa mbale ya Mtume wa
Allah Rehema na Amani zimshukie
akiwepo na Bi Maimuna (wote hawa ni wakeze) Akaja ibn Ummi Maktuum
na (tukio) hilo lilikuwa ni
baada ya kuamrishwa Hijaab Mtume akasema : “Jihifadhini nae”
tukamwambia : Ewe Mtume wa Allah,YEYE SI KIPOFU, HATUONI NA WALA
HATUJUI Mtume akasema :
“Je,
na nyinyi ni vipofu, hamuoni” Abuu Daawaoud na Tirmidhiy.
Kwa
hiyo haijuzu kwa wanawake “Ajnabiyaat”
kuangalia zaidi ya uso na vitanga kwa mwanaume “Ajnabiy” NA
WAAMBIE WAUMINI WA KIKE WAINAMISHE MACHO YAO NA WAZILINDE
TUPU ZAO………”(24: 31)
ii/.Ama
mwanamke mbele ya wanawake wenziwe
waislamu utupu wake ni sehemu yote ya mwili iliyo baina ya uso na kitovu
na mbele ya wanawake makafiri ni mwili wake wote ila sehemu inayodhihirika
kwa dharura wakati wa kufanya kazi za nyumbani
na nyingine kama hizo.
Mbele
ya wanaume maharimu zake ni
eneo lote lililo baina ya kitovu na magoti. Yaani
inajua kuwa wazi sehemu nyingine ya mwili isiyo hiyo tuliyoitaja
mbele ya naharimu zake lakini
kwa sharti ya kutokuzuka fitna. Ikiwa fitna haiaminiki basi si ruhusa
Tusome pamoja WALA
WASIONYESHE MAPAMBO YAO ILA KWA WAUME ZAO,AU BABA ZAO, AU BABA ZA WAUME
ZAO, AU WATOTO WAO, AU WATOTO WA WAUME ZAO, AU KAKA ZAO, AU WANA WA KAKA
ZAO, AU WANA WA DADA ZAO, AU WANAAKE WENZIO ( Waislamu) AU “(24:31)
Ama
mbele za wanaume “Ajaanibu” wa kando na kando : wasio waharimu zake ni
mwili wake wote Haijuzu kuonyesha sehemu yoyote ya mwili wake mbele yao ila kwa udhuru unaokubalika kisheria
haijuzu kwa wanaume hao
kumuangalia tusome:
“WAAMBIE
WAUMINI WA KIUME WAINAMISHE MACHO YAO (wasitazame yaliyokatazwa ) NA
WAZILINDE TUPU ZAO, HILI TAKASO KWAO…………24: 30
Imepokelewa
kutoka kwa Bi. Aysha- Allah amuwiye radhi
– amesema : Alikuwa Mtume wa Allah –Rehema
na Amani zimshukie- akiswali alfajiri basi
wakihudhuria pamoja nae (SWALA) wanawake waumini wakiwa
wamejiviringizia nguo zao Kisha (
Ibada ya swala ) hurejea majumbani mwao, hapana
yeyote aliyeweza kuwatambua (kutokana na namna walivyovaa)
Bukhaariy.
FAIDA
HALI/MAENEO AMBAYO KISHERIA INAJUZU KUFUNUA UTUPU NA KUUNGALIA
Inaruhusiwa
na sheria kufunua na kuuangalia
utupu kwa nyudhuru zifuatazo:
1
Wakati wa kuposa kwa lengo la kuoa.
Hapa mposaji anapewa ruhusa
na sheria kumtazama mwanamke
anayetaka kumposa .
Anachoruhusiwa
kuangalia ni uso na vitanga tu
na zoezi hili hufanyika mbele ya mawalii
wa binti sio faraghani baina ya wawili
hao peke yao.Tena ni kuangaliana tu
na sio kugusana.
2
Kutazama kwa ajili ya ushahidi au muamala.
Ili shahidi akubaliwe
Na
mahakama ya Kiislamu
kutoa ushahidi dhidi au
kwa mwanamke ni lazima anamtambua. Hapo ndipo sheria inampa ruhusa ya
kumuangalia uso tu. Eneo lingine ni pale
anapochanganyika na mwanamke huyo katika
shughuli fulani kama vile biashara au ajira pia ni lazima ajue
anafanya biashara na nani au
anamuajiri/anaajiriwa na nani.
Hapa pia anaruhusiwa kutazama uso tu.
3.
Kutazama kwa sababu ya kutibu na kufanya dawa. Mwanamke anaumwa,
Daktari ni mwanamume na hakuna daktari mwanamke.Sheria inamruhusu daktari kumuangalia popote
Mwanamke
huyo kwa lengo la tiba tu. Zoezi hili lifanyike mbele ya
maharimu wa mwanamke mgonjwa na sio
baina ya wagonjwa na daktari peke yao.
Imepokelewa
na Jaabir ibn Abdillah –Allah amuwiye radhi:- kwamba Umu Salamah Allah
amuwiye radhi – alimuomba Mtume wa Allah Rehema na Amani zimshukie ya
kupiga chuku.
Mtume
akamuamrisha Abu Twaybah ampige chuku “ Muslim”
CHUKU
(cupping) hii ni aina ya tiba inayohusisha ukataji wa mshipa maalum kwa
lengo la kutoa damu chafu
mwilini
Sharti
la nne itatajwa katika somo lijalo.
inshaallah
|