|
9.
KIKAO
CHA MWISHO.
Hapa
kinachokusudiiwa ni kile kitako kinachokuwa katika rakaa ya
mwisho ya
swala, kinachofandamiwa na salamu.
Ni
suna iliyothibiti
kukaa mkao wa “ Tawarruki”
katika kikao hiki cha
mwisho . Huu ni
mkao ambao mtu hukalia tako la kushoto
na sehemu
ya tako la kulia , akaunyoosha
mguu wa kulia kama unavyokuuwa katika si
jida na kuupitisha ule wa kushoto chini yake.
Imekuja
kaatika
riwaya ya Abuu
humayd : “ ……………..hata ilipokuwa sijida ambayo ndani yake
ndimo imo salamu ( sijida ya mwisho )
huutoa
mguu wake wa
kushoto na akakaa mkao wa tawarruki kwa kukalia tako lake la kushoto”
Abuu Daawound
10.
TASHAHUDI YA MWISHO { KATIKA KIKAO
CHA MWISHO}
Ni
wajibu kwa mwenye
kuswali akae
baada
ya sijda ya
mwisho ya swala yake asome “Tashahudi”
imepokelewa katika riwaya ya Ibn
Masoud Allah amuwiye radhi – amesema : Tulikuwa tukisema kabla ya
kufaradhishwa juu yetu Tashahudi
ASSALAAM
ALALLAH KABLA IBADIHI, ASSALAAM ALAA JIBRILL, ASSALAAM ALA MIIKAIL, ASSALAAM
ALA FULAN
Mtume
- Rehema na amani zimshukie
alipomalizaa kuswali alituelekkea , akatuambia “ Hakika
Allah ndiye AS – SALAAM , basi anapokaa mmoja wenu
katika
swala { Kwa
ajili ya Tashahudi } basi
na aseme
ATTAHIYYAAT
LILLAH WASSALAWATU WATTAYYIBAATU, ASSALAAM ALAYKA AYYUHA NNABII WARAHMATULLAH
WABARAKATUH, ASSALAAM ALAYNA WA-ALAIBADILLAHI SSALIHINA
Kwani
nyinyi mtakapoisema {salamu
hii}
humpata {humfikia} kila mja mwema mbinguni na ardhini.
Bukhaari na
Muslim.
Hili
ni mojawapo ya matamko
sahihi ya
Tashahudi ambayo
yaliyonukuliwa kutoka kwa Bwana
Mtume. Tashahudi yeyote iliyothibiti kutoka kwa Mtume mtu
akiisoma itamjuzia.
Sharti
za Tashahudi.
Msomaji
wa Tashahudi analazimika kuchunga yafuatayo:
-
Ajisikizishe
yeye
mwenyewe matamko ya Tashahudi
iwapo hana tatizo la kusikia.
-
Kukifululiza
kisomo cha tashahudi, yaani asiweke mwanya mkubwa baina ya ibara za
Tashahudi . pia asitie kati dhikri nyingine , akifanya hivyo yaani
akinyamaza kinyamao kirefu au
akilia kati dhikhri
nyingine , Tashhahudi yake
itakuwaa imebatilika na itamuwajibikia kuianza upya.
-
Aisome
katika hali ya kukaa isipokuwa katika mazingira ya dharura tu ndio
anaruhusiwa kuisoma
katika hali
yoyote imkinikiayo.
-
Aisome
kwa lugha ya
Kiarabu . Akishindwa atasoma tafsiri yake kwa Lugha
yake, Lakini bado atakuwa na wajibu wakujifunza mpaka aweze kuisoma
kiarabu kama alivyofanya Mtume wa Allah- Rehema na Amani zimfikie.
-
Achunge
matokeo ya herufi , shada na hukumu zote za usomaji . akifanya kosa
lolote litakalopelekea
kuharibika
kwa maana,
halitamaanisha zaidi ya
kubahatilika Tashahudi yake
hiyo . Kwa
hivyo basi itamlazimu kuirejea upya .
-
Ayatungamanishhe
maneno ya Tashahudi
kwa mtungo wake kama yalivyopokelewa kutoka kwa Mtume wa Allah –
Rehema na Amani
zimshukie .
|