|
SWALI: Riba tunayo pewa kwa
kuweka pesa zetu katika mabenki ya riba,
hatuitumii kwa kuwa ni haramu. Je, tuendelee
kuyaachia mabenki hayo au tuichukue na kuitumia
katika maslahi ya Waislamu?
JIBU: Katika mas-ala haya,
wanachuoni wetu-Allah awarehemu-wamesema: Mwenye
kuwa na mali ya haramu, ni wajibu ajitakase nayo
kwa namna/sura ambayo hatonufaika nayo yeye
binafsi. La si katika kujivutia maslahi yeye,
kama vile kutumia katika kula, kunywa, maskani,
matumizi ya familia, karo ya shule na kadhalika.
Na wala sio katika kujiondoshea madhara au
dhuluma, kama vile kutumia katika gharama za
bima ya lazima au baki ya aina nyingine za kodi
na ushuru. Na wakati wa kuitoa mali haramu hiyo,
nia iwe ni kujitakasa nayo na sio sadaka, kwa
sababu Allah ni Mzuri hakipokei ila kilicho
kizuri (cha halali).
Ama uringo ambamo hutumiwa humo
mali za riba, huwa ni katika njia mbali mbali za
kheri, mfano: Kuwapa mafakiri na masikini,
gharama za matibabu kwa wahitaji, wenye madeni,
harakati za vituo vya Kiislamu na kama haya.
Mali haramu, huwa ni haramu kwa
mchumaji wake. Ama kwa mwenye kupewa, kunamjuzia
kufaidika nayo na kwake huzingatiwa kama mali
iliyo potea, isiyo na mwenyewe.
Allah ndiye Mjuzi mno. |