|
SWALI: Nini hukumu ya udhu kwa
mwanamke aliye zitia kucha zake hiki kinacho
itwa leo “rangi ya kucha”?
JIBU: Hakujuzu kwa mwanamke
anaye swali kupaka rangi kucha zake ikiwa rangi
hiyo inayazuia maji kukufikia kiungo wakati wa
kuchukua twahara ya udhu au josho. Na kila kitu
kinacho zuia maji kufika kwenye kiungo kinacho
twaharishwa, hakijuzu kutumiwa na mwenye
kutawadha au mwenye kuoga, kwa sababu Allah
Ataadhamiaye anasema: “...BASI OSHENI NYUSO
ZENU, NA MIKONO YENU...” [05:06]
Na mwanamke akiwa amezipaka
rangi kucha zake, bila ya shaka rangi hiyo
inayazuia maji kukifikia kiungo kinacho oshwa,
kwa ajili hiyo basi anakuwa bado hajauosha mkono
wake. Na kwa kitendo chake hicho cha
kutokukamilisha kuosha kiungo cha udhu, anakuwa
ameiacha mojawapo ya nguzo za udhu/josho.
Allah ndiye Mjuzi mno. |